Home Habari za michezo BACCA SASA KUTOKA LIGI KUU MPAKA ULAYA

BACCA SASA KUTOKA LIGI KUU MPAKA ULAYA

Habari za Yanga SC

Kwa sasa hapa nchini Ibrahim Bacca ni miongoni mwa mabeki bora wa kati wa Ligi Kuu na hata ukiweka orodha ya mabeki watatu bora basi huwezi kuacha kuweka jina lake.

Tangu asajiliwe na Yanga akitokea KMKM ya Zanzibar kiwango chake kimeendelea kukua maradufu na kupata nafasi ya kuitwa timu ya Taifa. Januari mwakani atakwenda AFCON yake ya kwanza pale nchini Ivory Coast.

Kwa sasa ana miaka 25 huu ndio wakati wake wa kwenda Ulaya kutafuta malisho mazuri zaidi ya anachokipata pale Yanga. Ni wakati sasa wanaomsimamia wamtafutie timu hata daraja la pili Ufaransa au kule katika Ligi kuu za Ulaya Mashariki.

Ibrahim Bacaa amekuwa bora mbele ya Bakari Mwamnyeto na Dickson Job ndio maana hata Kocha Miguel Gamondi huwa anamtumia Bacca kucheza na hawa wawili ila sio kuanza nje.

SOMA NA HII  KWA MKAPA LEO VITA YAO ITAKUWA NAMNA HII