Home Habari za michezo HIZI HAPA PONGEZI ZA AHMED ALLY KWA YANGA….

HIZI HAPA PONGEZI ZA AHMED ALLY KWA YANGA….

Habari za Michezo leo

Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally amewapongeza watani zao Yanga SC kwa hatua waliofikia kwenye mchakato wao wa ujenzi wa Uwanja makao makuu Jangwani.

“Mimi kama Ahmed Ally ningependa kuona Yanga SC wanakajenga uwanja kwasababu tunayo changamoto kubwa ya viwanja kwahiyo klabu ikijikwamua na kujenga uwanja wake ni jambo la kupongezwa.

“Kwa sasa tuwaache wajenge huu uwanja hizi ramani, mpango mkakati tumeshazishuhudia sana baada ya hapo tutaanza kujadili jukwaa flani liitwe jina gani kwa sabu tukiangalia pale Jangwani uwanja utaenda na maji.

“Nimemskia Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Albert Chalamila akilaumu waliojenga stendi pale Jangwani, sijajua kuhusu uwanja,” amesema Ahmed Ally.

SOMA NA HII  KUHUSU USAJILI MPYA MSIMBAZI..SENZO EMEFUNGUKA HAYA..!!