Home Habari za michezo AMSHA AMSHA ZA KOMBE LA YANGA LEO HUU HAPA🔥🔥SKUDU KAMA KABEBA KOMBE...

AMSHA AMSHA ZA KOMBE LA YANGA LEO HUU HAPA🔥🔥SKUDU KAMA KABEBA KOMBE LA DUNIA VILE 😂😂..

Habari za Yanga leo

DAR ES SALAAM ni kijani na njano hakuna rangi ambayo imetawala katika jijj hili zaidi ya hizo mbili, hao ni Yanga ambapo leo waliweza kutembeza kombe lao la ubingwa wao wa 30 waliotwaa msimu huu.

Kombe hilo walikabidhiwa jana baada ya mchezo na Tabora United uliochezewa uwanja wa Benjamin Mkapa ambapo Yanga waliuibuka na ushindi wa mabao 3-0.

Habari za Yanga leoYanga walianza sherehe zao kuanzia mapema  saa 4:00 asubuhi kwa mashabiki wao kunywa supu uwanja wa Benjamin Mkapa, ambapo kulianzia shamra shamra za kusherehekea Ubingwa wao.

Baada ya kunywa supu wachezaji na baadhi ya viongozi walipanda kwenye basi maalum ambalo limebeba kombe lao la ubingwa huku wakifunga baadhi ya barabara kwa sababu ya kulitembeza kombe lao kutoka uwanja wa Benjamin Mkapa.

Habari za Yanga leoWalipita Keko, Tazara, Buguruni, Karume. Mitaa ya Msimbazi na safari kuishia makao makuu ya klabu hiyo huku maelfu ya mashabiki wamejitokeza kwenye Paradi hiyo.

Ndani ya saa tatu na nusu zilitumika kufanya Paradi hiyo kutoka Uwanja wa Benjamin Mkapa hadi makao makuu wa klabu hiyo ambapo wamefika Saa 7: 30 makao makuu ya klabu hiyo .

Habari za Yanga leoWalipowasili makao makuu ya klabu hapo Ofisa habari wa Yanga, Ali Kamwe ametambulisha benchi la ufundi linaloongozwa na Kocha Mkuu, Miguel Gamondi na viongozi wa kamati ya utendaji inayoongozwa na Rais Hersi Said.

Baada ya hapo wakatambulishwa baadhi ya Mashujaa wao ambao wamefanikiwa kutetea taji lao kwa mara ya tatu na kufanikiwa kwenda kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika kwa msimu mwingine.

Habari za Yanga leoNahodha Msaidizi wa Yanga, Dickson Job amesema anawashukuru wanachama na mashabiki wa Yanga kuwa pamoja nao kwa msimu mzima na kuendelea  kuwasapoti katika michezo iliyosalia.

“Bado hatujamaliza na tunakibarua kingine mbele yetu, tuna deni lingine na tunatakiwa kwenda kulilipa visiwani Zanzibar, katika fainali ya kombe la Shirikisho la CRBD Bank kwa kurejea Dar es Salaam na kombe, alisema Job na kuwataka mashabiki kuendelea kuwasapoti katika safari yao hiyo,” amesema Job

Naye Rais wa Yanga, Hersi amesema wachezaji , benchi la ufundi na uongozi wamefanya kazi kubwa ya kuchangia ubingwa wa 30 na mara ya tatu na kufanikiwa kuwa mali yao.

Habari za Yanga leo“Kila mmoja anatambua kuwa Juni 2, mwaka huu kuna kibarua kigumu sana mbele yetu na tunaenda kupambana kuhakikisha tunafanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Shirikisho na kuja kulitambulisha kwa mara nyingi hapa klabuni.

Niwaahidi mashabiki na wanachama tunaenda kujenga timu yetu bora kuliko msimu huu kwa kusajili nyota wengine wenye uwezo na hatutaacha mchezaji yoyote yule ambaye atakuwa kwenye mipango yetu,” amesema Hersi.

SOMA NA HII  WAKATI CHAMA AKIIRUDISHA SIMBA KWENYE SAYARI YAKE...BOCCO MAMBO YAZIDI KUWA MAGUMU..UKWELI UKO HIVI..