Home Habari za Simba Leo KUHUSU USAJILI WA JOBE MANGUNGU AFUNGUKA A-Z….MIL 700 TZS

KUHUSU USAJILI WA JOBE MANGUNGU AFUNGUKA A-Z….MIL 700 TZS

UNAMKUMBUKA PAR OMAR JOBE? Strika la Magoli aliyeshindwa kufanya maajabu ndani ya Mitaa ya Maimbazi, tangu atue Simba katika dirisha dogo.

Mwenyekiti wa klabu ya Simba Murtaza Mangungu amesema kwamba hawafikirii kuachana na mchezaji Par Omar Jobe kwani ni mchezaji mzuri.

Murtaza Mangungu alizungumza hayo kupitia Clouds FM, alipokuwa akifafanua juu ya masuala mbalimbali yanayoendelea kwa sasa ndani ya klabu hiyo.

“Mkataba wa Jobe ni mrefu kidogo sidhani kama tutaweza kuuvunja, kwanza sio mchezaji mbaya ni mchezaji mzuri na nilimtembelea, tumezungumza na tutaendelea na mchakato wa kuimarisha kiwango chake.” — Murtaza Mangungu.

Mkataba wa Par Omar Jobe ili kuuvunja klabu ya Simba inapaswa kulipa fidia ya Tsh Milioni 700, kwani alisajili kwa miaka miwili na hadi wakati huu ametumikia mkataba wake kwa miezi 6 pekee.

Kuhusu usajili wa Ismael Sawadogo pia ambaye ni mchezaji aliyeshindwa kuonesha kiwango kizuri, na kupelekea kuachwa na Simba Mangungu alisema;

“Yeye amezungumzia wachezani wawili Sawadogo na Jobe , bahati mbaya Sawadogo wakati anakuja pre season aliumia , lakini alikuwa anatoka kwenye timu yao ya Taifa sio mchezaji wa kiwango kidogo”

“Mimi ninachosema hapa atokee mtu anipe timu 5 ambazo wamesajili na wachezaji wote waliosajiliwa wamefanya vizuri,Wallah mimi wala sisubiri kitu ,kesho najiuzulu”

Kinacho endelea katika klabu ya Simba, wanachama ba mashabiki wanashinikiza Mangungu na wajumbe wake wajiuzulu, hivyo kinachotakiwa ni kuitishwa kwa Mkutano Mkuu wa Dharula kama ambavyo katiba ya Simba inasema.

SOMA NA HII  KOCHA SIMBA ATUMA SALAM YANGA...FADLU AIREJESHA HESHIMA YA MNYAMA