YANGA Imejipanga kushinda ushindi mkubwa zaidi kwenye mechi ya marudiano dhidi ya Vital ‘O katika uwanja wa Azam Complex Chamazi.
Mlinda mlango wa klabu hiyo AbdulTwalib Mshery alisema kwamba wachezaji wenzake na yeye wanafahamu jukumu kubwa lililopo mbele yao, na hivyo wamejipanga vizuri kuhakikisha wanashinda.
“Tutafuata maelekezo ya mwalimu kama ambavyo atatuelekeza. Hatufikiri mechi iliyopita, tunatazama mchezo ujao. Mchezo unaokuja kwetu ni kama tunaanza upya bila kujali yaliyotokea.