MUVI YA SIMBA NA OKWI YAJA NA JINGINE JIPYA
Habari za ndani zinasema kwamba Kaizer Chiefs ina asilimia 85 za kumnasa Emmanuel Okwi, lakini Simba wamecharuka na kujipanga kivingine. Simba imeapa kwamba hata kwa kulipa faini ya kuchelewa lazima wahakikishe Okwi anabaki Msimbazi na wataelewana tu ingawa anawapiga chenga.Okwi kwa sasa yupo na Uganda kwenye Afcon na inadaiwa kwamba ameshasaini mkataba wa awali na Kaizer ambayo imeshamsainisha kiungo...
AJIBU KUFURU SIMBA, KULIPWA TSH.MIL 1,250,000 KWA WIKI
Lanchi ya juzi haikuwa na raha kwa mashabiki wa Yanga, baada ya Simba kumtambulisha rasmi Ibrahim Ajibu kwamba amerejea Msimbazi.Simba imemfanyia kufuru nahodha huyo wa Yanga ambapo kila sekunde atakayokuwa akipumua hata kama atakuwa amelala nyumbani kwake watamlipa Sh116. Iko hivi dau lake la usajili alilokunjia mfukoni katika mkataba wa miaka miwili ni Sh.mil 80.Mshahara wake kwa mwezi ni...
JESHI LA SIMBA KUTUA KWA MANDELA
Kocha wa Simba, Patrick Aussems anatua nchini wiki ijayo na timu inakwenda kambini nchini Afrika Kusini.Habari za uhakika zinasema kwamba, Simba ilikuwa na mpango wa kwenda Ulaya lakini mpaka sasa wengi wanapendekeza Sauzi ndiyo sehemu nzuri na ina vifaa vyote ambavyo vinastahili kwa kambi ya kiwango cha Simba.Katibu wa Simba, Dkt Anorld Kashembe alisema mpango wa kambi yao ni...
KAHATA WA SIMBA AMECHEMSHA
Kocha wa Kenya, Sebastian Migne amekiri kwamba staa mpya wa Simba, Francis Kahata hakuwa na bahati kwenye Afcon ya msimu huu.Migne amekiri kwamba hata kwenye mechi na Tanzania hakuwa na wakati mzuri ingawa inawezekana alipania sana. Hata kwenye mechi na Algeria mchezaji huyo alitolewa mapema baada ya kushindwa kuhimili mchezo.Kocha huyo anasema kwamba Kahata ni miongoni mwa mastaa ambao...
ZAHERA ASHINDWE MWENYEWE TU
UONGOZI wa Klabu ya Yanga umefunguka kuwa kwa asilimia 90 umefanikiwa kukamilisha usajili aliokuwa akiutaka Kocha Mwinyi Zahera baada ya kusajiliwa wachezaji aliowapendekeza.Aidha, kabla ya Zahera kwenda kuitumikia timu yake ya Taifa ya DR Congo katika Michuano ya Afcon 2019, alitoa mapendekezo yake juu ya wachezaji ambao anawahitaji kwa ajili ya msimu ujao jambo ambalo uongozi huo umeeleza kulifanyia...
AJIBU AKATAA JEZI SIMBA
AJIBU ameliamsha Msimbazi baada ya kugomea kukabidhiwa jezi namba 23.Namba hiyo 23 ilikuwa inavaliwa na kiungo huyo mtaalam wa assisti, awali akiwa anaichezea Simba kabla ya kutua Yanga msimu wa 2017/2018 kama mchezaji huru.Inasemekana kuwa, Ajibu alishasaini mkataba wa miaka miwili muda mrefu kabla ya kutambulishwa jana wakati wa lanchi baada ya mkataba wake kumalizika rasmi juzi Jumatatu.Kwa mujibu...
YANGA WAMTAJA MBADALA WA GADIEL MICHAEL
UONGOZI wa Yanga umesema kuwa kwa sasa hauna papara na mchezaji wa kikosi hicho Gadiel Michael ambaye amegoma kusaini ndani ya klabu hiyo.Mwenyekiti wa Yanga Mshindo Msolla amesema kuwa kwa sasa Yanga imefanya usajili wa maana hivyo hawawezi kusumbuliwa na mchezaji mmoja."Tumefanya usajili makini msimu huu, kama mabeki tunao mtu kama All Sonso na Ally Ally hawa wote wapo...
NAHODHA WA TIMU YA TAIFA AJIVUNIA UWEZO WA WACHEZAJI WENZAKE
NAHODHA wa timu ya Tanzania, Mbwana Samatta amesema kuwa licha ya kupoteza michezo yote waliyocheza kwenye michuano ya Afcon bado anajivunia uwezo wa wachezaji wenzake.Stars imetolewa kwenye michuano ya Afcon baada ya kucheza michezo yote mitatu bila kujikusanyia pointi huku ikikubali kufungwa jumla ya mabao nane na kufunga mabao mawili pekee."Haikuwa lengo letu kufanya vibaya, tulipambana kwa kadri ya...
PAUL POGBA AIKAZIA MANCHESTER UNITED, KUOMBA ASEPE ZAKE MSIMU UJAO
IMERIPOTIWA kuwa Paul Pogba kiungo wa Manchester United ana mpango wa kuwaomba mabosi zake wampe ruhusa ya kuondoka ndani ya kikosi hicho kabla hawajafanya ziara ya kwenda Australia.Pogba kwa sasa amekuwa hana mpango wa kubaki ndani ya United baada ya kusema kwamba anahitaji kupata changamoto mpya nje ya kikosi hicho.Real Madrid na timu yake ya zamani ya Juventus zote...
WALTER BWALYA AIPA TANO SIMBA KWA KAHATA
BAADA ya kusaini kandarasi ya miaka miwili ndani ya Simba, kiungo Francis Kahata ambaye ametoka timu ya Gormahia mshambuliaji wa Nkana FC, Walter Bwalya amesema kuwa anamtambua vema Kahata amekuja kufanya kazi mashabiki watampenda.Kahata ambaye ni nyota ndani ya kikosi cha timu ya Taifa ya Kenya kwa sasa ni mali ya Simba."Namtambua Kahata ni mtu wa namna gani hivyo...