Home Uncategorized FIFA KUMPA TUZO YA HESHIMA NYOTA WA ZAMANI WA TIMU YA TAIFA...

FIFA KUMPA TUZO YA HESHIMA NYOTA WA ZAMANI WA TIMU YA TAIFA YA CAMEROON

ALBERT Roger Mooh Milla, Septemba 7 atapewa tuzo na Shirikisho la Soka Duniani (Fifa) kwa kufunga bao akiwa na miaka 42.

Mpaka sasa imeshapita miaka 20 tangu nyota huyo apachk bao hilo kwenye michuano ya Kombe la Dunia.

Bao hilo alifunga kwenye mchezo wa timu yake ya Taifa ya Cameroon dhidi ya Urusi mwaka 1994 na kwa sasa ana umri wa 67

Tuzo hiyo itakuwa ni ya mfungaji mwenye umri mkubwa zaidi katika Kombe la Dunia na itatolewa Septemba 7 nchini Sweden.


Kwenye mchezo huo ambao ulichezwa uwanja wa Stanford nchini Marekani, Cameroon ilipoteza kwa kufungwa mabao 6-1 na timu ya Urusi ambayo nayo ilikuwa imeshatolewa kwenye michuano hiyo mikubwa.

SOMA NA HII  HIKI NDICHO KIWANGO CHA MISHAHARA KWA WACHEZAJI SIMBA, NI BALAA ZITO