Home Uncategorized MAKATA ALIYEZIPANDISHA ALLIANCE FC NA POLISI TANZANIA APEWA TIMU YA DODOMA

MAKATA ALIYEZIPANDISHA ALLIANCE FC NA POLISI TANZANIA APEWA TIMU YA DODOMA

MBWANA Makata ameteuliwa kuwa Kocha Mkuu wa Dodoma FC inayoshiriki Ligi Daraja la kwanza.

Godwin Kunambi ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma amemtambulisha Kocha huyo na kusema kuwa lego kuu la timu ni kujinasua kutoka hatua ya Daraja la Kwanza mpaka kufika Ligi Kuu Bara.

“Tutampa ushirikiano Kocha Makata katika kila jambo na kufanya usajili kwa mchezaji yoyote ambaye tutakuwa tayari kutoa pesa ili ajiunge na timu yetu,” amesema.

Miongoni mwa timu ambazo Makata alizipandisha Daraja ni pamoja na Alliance FC iliyo chini ya Malale Hamsini, Polisi Tanzania ambayo kwa sasa ipo chini ya Kocha Seleman Matola.

SOMA NA HII  MUONEKANO WA UKURASA WA NYUMA GAZETI LA CHAMPIONI IJUMAA