PATRICK Aussems, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa uwezo wa wachezaji wa Simba unaongezeka kila siku hivyo anaamini wataleta ushindani msimu ujao.
Simba imeweka kambi nchini Afrika Kusini kwa ajili ya maandalizi ya ligi kuu pamoja na michuano ya kimataifa.
“Wachezaji wapo vizuri na wanaendelea vizuri hivyo imani yangu ni kuona kila mmoja anafanya kile ambacho nimemuelekeza.
“Ugumu mkubwa upo msimu ujao hasa ukizingatia ratiba imebana kuliko kawaida nasi tunapaswa tufanye vizuri pia,” amesema.
Simba inatarajia kurejea Bongo Julai 31 baada ya kumaliza maandalizi yao ambayo yatatumia wiki mbili.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.