Home Uncategorized KMC: AS KIGALI TUNAWAMUDU KABISA

KMC: AS KIGALI TUNAWAMUDU KABISA


JACKSON Mayanja, Kocha Mkuu wa timu ya KMC amesema kuwa kikosi chake kipo tayari kwa ajili ya michuano ya kimataifa.


KMC itamenyana na AS Kigali ya Rwanda Agosti 10 mchezo wa kwanza wa kombe la Shirikisho kwa sasa wanafanya mazoezi uwanja wa Bora kujiweka sawa.

Amosi Charse beki kulia wa KMC amesema kuwa mazoezi wanayoyapata yanawapa imani ya kufanya vizuri kwenye mchezo wao dhidi ya AS Kigali.

“Tunaendelea vema na mazoezi na tupo sawa kwa ajili ya ushindani, ahadi yetu ni kufanya vizuri na kupata ushindi mbele ya AS Kigali kwani tunawamudu,”amesema.
SOMA NA HII  MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA CHAMPIONI JUMATANO