Home Uncategorized KOCHA YANGA:MOLINGA ATAFUNGA MABAO MENGI

KOCHA YANGA:MOLINGA ATAFUNGA MABAO MENGI



LUC Eymael, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa anaimani mshambuliaji wake David Molinga atafunga mabao mengi kwenye ligi.

Molinga ni kinara ndani ya Yanga akiwa ametupia jumla ya mabao saba kati ya 25 ambayo yamefungwa na Yanga. Akizungumza na Saleh Jembe, Eymael amesema kuwa ana imani na Molinga akiendelea na kasi yake atafunga mabao mengi.

“Molinga anashindwa kutulia akiwa ndani ya 18 na uwanjani pia ila akipata nafasi anafunga, endapo atafanyia kazi makosa yake ana nafasi ya kufunga mabao mengi msimu huu,” amesema.

SOMA NA HII  SPURS WAENDELEZA MAKALI,KANE NA SON NI HABARI NYINGINE