Home Uncategorized NCHIMBI AFICHUA ALICHOAMBIWA NA MZUNGU ILI AITUNGUE ALLIANCE

NCHIMBI AFICHUA ALICHOAMBIWA NA MZUNGU ILI AITUNGUE ALLIANCE


DITRAM Nchimbi, mshambuliaji wa Yanga amesema kuwa Kocha Mkuu Luc Eymael alimwambia kuwa akatumie makosa ya wapinzani ili akaifungie timu yake mabao.

Jana, Februari 29, Yanga ilishinda mbele ya Alliance mabao 2-0 na kuifanya ifikishe pointi 44 ikiwa nafasi ya nne kwenye msimamo.

Nchimbi amesema:”Mwalimu aliniambia kwamba ninapaswa nitazame mapungufu ya wenzangu na nikafunge ili kuipa timu ushindi na mwisho wa siku ndicho kilichotokea,”.

Yanga imeipiga nje ndani Alliance kwani mchezo wa kwanza uliochezwa CCM Kirumba ilishinda kwa mabao 2-1 na jana imeshinda mabao 2-0.

SOMA NA HII  KUHUSU MSIMU UJAO....BEKI YANGA AITAJA SIMBA..!!!