Home Uncategorized PAMBA YAPOTEZA MBELE YA GEITA GOLD

PAMBA YAPOTEZA MBELE YA GEITA GOLD

NYOTA wa Geita Gold inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza, George Mpole jana aliisepa na mpira wake baada ya kuitungua mabao matatu timu ya Pamba SC ya Mwanza.

Mchezo huo uliochezwa jana, Februari 9,2020 ulichezwa Uwanja wa Nyankumbu.

Kwa sasa Geita Gold ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 25 baada ya kucheza mechi 14 huku Pamba ikiwa nafasi ya 12 na pointi zake 14.

Kwenye kundi B kinara ni Gwambina ambaye amejikusanyia jumla ya pointi 28 na imecheza mechi 14.

SOMA NA HII  HIVI NDIVYO HASIRA ZA SIMBA KUFUNGWA NA YANGA ZILIVYOKUTANA NA SINGIDA UNITED UHURU