Home Uncategorized SIMBA: HAKUNA MUDA WA KUPUMZIKA, KAZI JUU YA KAZI

SIMBA: HAKUNA MUDA WA KUPUMZIKA, KAZI JUU YA KAZI

GADIEL Michael, beki wa Simba amesema kuwa kwa sasa mapambano lazima yaendelee kwani hakuna muda wa kupumzika kwenye maisha ya soka.

Michael alipewa nafasi ya kuvaa kitambaa cha unahodha kwenye mchezo wa hatua ya 16 bora Kombe la Shirikisho mbele ya Stand United mchezo uliochezwa Februari 25 Uwanja wa Kambarage, Shinyanga na Simba ilishinda kwa penalti 3-2 baada ya dakika 90 kutoshana nguvu kwa sare ya kufungana bao 1-1.

Michael amesema:”Hakuna muda  wa kupumzika ni lazima kupambana ili kuwa bora na kufikia malengo ambayo tumejiwekea kazi bado inaendelea na kila kitu kinakwenda sawa.

“Yote ambayo yanatokea kwenye soka yanabebwa na nidhamu, kujituma na kushirikiana na wenzangu,”.

SOMA NA HII  AZAM FC V SIMBA NI VITA YA KISASI LEO