KIKOSI cha Simba, jana kimefanya mazoezi ya mwisho kwa ajili ya kumalizana na Azam FC kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa leo Uwanja wa Taifa majira ya saa 1:00 usiku.
Azam wataikaribisha Simba wakiwa wamefanya mabadiliko kwenye uongozi wao ikiwa ni pamoja na kuachana na Kocha Msaidizi Idd Cheche pamoja na Ofisa Habari, Jaffary Maganga.
Simba itaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu za kushinda bao 1-0 mchezo wa kwanza walipokuwa nyumbani uwanja wa Taifa.
Bao hilo la ushindi lilifungwa na Meddie Kagere hivyo leo kazi itakuwa ni moja kwa timu ya Azam kulipa kisasi huku Simba ikihitaji kulinda rekodi.
Azam FC ipo chini ya Arstica Cioaba jana ilifanya pia mazoezi ya mwisho kumalizana na wapinzani wao Simba.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.