KOCHA Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck amesema kuwa wapo tayari kusepa na pointi tatu muhimu mbele ya Mtibwa Sugar leo Uwanja wa Jamhuri.
Sven raia wa Ubelgiji mchezo wake uliopita Uwanja wa Uhuru alichapwa bao 1-0 na JKT huku Mtibwa Sugar iliyo chini ya Zuber Katwila ikipoteza mbele ya Lipuli kwa kufungwa bao 1-0 Uwanja wa Ghairo.
Mbelgiji huyo amesema kuwa kila kitu kipo sawa ana matumaini yake ni kupata pointi tatu muhimu.
“Wachezaji wana morali kubwa na kila kitu kipo sawa imani yangu ni kuona tunafikia malengo ya kupata pointi tatu muhimu,” amesema.
Simba ipo nafasi ya kwanza baada ya kucheza mechi 20 imefikisha jumla ya pointi 50.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.