Home Uncategorized TANZANIA PRISONS KUINGIA KWA TAHADHARI MBELE YA AZAM FC

TANZANIA PRISONS KUINGIA KWA TAHADHARI MBELE YA AZAM FC

ADOLF Rishard, Kocha Mkuu wa Tanzania Prisons amesema kuwa ataigia kwa tahadhari mbele ya Azam FC kwenye mchezo wao wa leo, Februari 5, wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa Uwanja wa Taifa majira ya saa 10:00 Jioni.

Rishard ambaye aliongoza timu yake kucheza mechi 12 bila kupoteza amesema kuwa amewajenga wachezaji wake kisaikolojia jambo liakalowafanya waendelee kupambana kurejea kwenye mstari.

“Tulipoteana hivi karibuni mara baada ya kufungwa na Yanga ila hilo halitupi shida kwa kuwa nimeongea na vijana wangu na wameahidi kuendelea kufanya kazi kweli, ninatambua tuna mechi nyingi nzuri na ngumu tutapambana kupata matokeo na tutawafuata wapinzani weu kwa tahadhari,” amesema.

SOMA NA HII  SIMBA KUIFUATA MBEYA CITY LEO