Home Uncategorized YANGA:TUNAZITAKA POINTI TATU ZA COASTAL UNION

YANGA:TUNAZITAKA POINTI TATU ZA COASTAL UNION


LUC Eymael, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa leo watapambana mbele ya Coastal Union kupata pointi tatu muhimu kwenye mchezo wao wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Eymael amekiongoza kikosi chake kusepa na pointi tatu kwenye mechi tatu baada ya kulazimisha sare tatu mfululzio ndani ya dakika 270.Mchezo wake uliopita alikubali sare ya kufungana bao 1-1 na Polisi Tanzania Uwanja wa Ushirika.

Leo atakutana na Coastal Union ya Juma Mgunda iliyotoka kuchapwa mabao 2-1 na Ruvu Shoting.

Eymael amesema:-“Mchezo muhimu na mkubwa kwetu, tumejipanga kuona namna gani tunapata pointi tatu, wachezaji wapo tayari nasi tupo tayari, mashabiki watupe sapoti,”.

Mbeya City, Tanzania Prisons na Polisi Tanzania walikaza walipkutana na Yanga na kugawana pointi mojamoja.

SOMA NA HII  HII HAPA RATIBA YA MECHI 10 ZA SIMBA ZILIZOBAKI