Home Uncategorized HIVI NDIVYO NYOTA WA KAGERA SUGAR ANAVYOLINDA KIPAJI CHAKE NA KUCHUKUA TAHADHARI

HIVI NDIVYO NYOTA WA KAGERA SUGAR ANAVYOLINDA KIPAJI CHAKE NA KUCHUKUA TAHADHARI

YUSUPH Mhilu, nyota wa timu ya Kagera Sugar amesema kuwa kwa sasa anaendelea na mazoezi ya kulinda kipaji chake ili kuwa bora endapo Ligi Kuu Bara itarejea.

Kwa sasa ligi imesimamishwa kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona ambapo tamko hilo lilitolewa Machi 17 kupitia kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mhilu amesema kuwa anaendelea kufanya mazoezi na kuchukua tahadhari kwa ajili ya kujilinda dhidi ya Virusi vya Corona.

“Bado hali sio shwari kwa sasa dua ni muhimu ili kila kitu kirejee kama zamani na maisha yaendelee kikubwa ni kuona namna gani tunaweza kujilinda na kuchukua tahadhari.

“Kwa sasa bado ninaendelea kufanya mazoezi ili kulinda kipaji changu na kuchukua tahadhari kwa ajili ya kujilinda dhidi ya Virusi vya Corona,” amesema.

Mhilu ametupia mabao 11 ndani ya Ligi Kuu Bara na ametoa pia pasi mbili za mabao.

SOMA NA HII  CHAMA AMKOSHA KOCHA WA NAMUNGO