Home Uncategorized MKALI WA PASI ZA MWISHO YANGA AFICHUA KILICHO NYUMA YA KUPETA KWAKE

MKALI WA PASI ZA MWISHO YANGA AFICHUA KILICHO NYUMA YA KUPETA KWAKE

JUMA Abdul, nahodha msaidizi wa Yanga amehusika kwenye mabao matano kati ya 31 yaliyofungwa na Yanga kwenye Ligi Kuu Bara.

Abdul ametoa pasi tano ndani ya Yanga na anaongoza kwa kutoa pasi za mwisho.

Beki huyo amesema kuwa sababu kubwa ya kurejea kwenye kiwango chake ni mazoezi na juhudi isiyo ya kawaida. 

“Kikubwa ni mazoezi na juhudi katika kile ambacho ninakifanya kwa kuwa ni kazi yangu na ninaipenda,” amesema.

Kwa sasa Ligi Kuu Bara imesimama kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona ambalo ni janga la dunia.

SOMA NA HII  NYOTA WA SIMBA KUTIMKIA SINGIDA UNITED