Home Uncategorized KUHUSU GADIEL MICHAEL NA ZIMBWE NDANI YA SIMBA SOMO LIPO HIVI

KUHUSU GADIEL MICHAEL NA ZIMBWE NDANI YA SIMBA SOMO LIPO HIVI


GADIEL Michael Mbaga alitua Simba kama sahihisho la Mohammed Hussein Zimbwe kwa maana ya kuwa akionekana ni bora kwa mambo kadhaa.

Wakati anatua Simba, Zimbwe amekuwa bora zaidi, kwa sasa ni namba tatu kwa kiwango bora na anafanya vizuri.

Maana yake, Gadiel analazimika kuanza kupigania namba upya licha ya kwamba alikuwa tegemeo Azam FC na Yanga.

Mpira ndio uko hivi, unataka mapambano kila kukicha na lazima uendelee kujituma ili upate namba na ukipata ujitume kubaki nayo.

Hawa wote ni vijana wa kitanzania wanaopambana na maisha na nia yao ni kujijenga na hakuna ubishi wote ni mabeki wazuri lakini katika maisha, mapambano ni muhimu.

Huu ni mfano mzuri wa maisha kwamba mambo mazuri yanapatikana kupitia Juhudi na Maarifa, yanatofuata yanakuwa ni nyongeza.

SOMA NA HII  SIMBA YATOA SOMO HILI KUHUSU CORONA KWA WATANZANIA