Home Uncategorized YANGA YAFICHUA SIRI YA USHINDI KWA ALLIANCE

YANGA YAFICHUA SIRI YA USHINDI KWA ALLIANCE

KOCHA Mkuu wa Yanga, Luc Eymael amesema kuwa siri kubwa ya ushindi wa mabao 2-0 mbele ya Alliance ni wachezaji wake kufuata maelekezo aliyowaambia mwanzo na juhudi zao binafsi.

Yanga ilishinda mbele ya Alliance na mfungaji wa mabao akiwa ni Ditram Nchimbi aliyefunga mabao hayo yalioipa pointi tatu Yanga.

Eymael amesema:”Kazi ya wachezaji ilikuwa kubwa na kila mmoja ametimiza majukumu yake nina amini kwamba kazi niliyowapa wameitimiza na kufuata maelekezo niliyowapa ndio kilichobeba ushindi wetu,”.

Yanga inafikisha pointi 44 ikiwa nafasi ya nne na imecheza mechi 23 ndani ya ligi.

SOMA NA HII  MBELGIJI WA YANGA AACHIWA KAZI YA KUCHAGUA WACHEZAJI ANAOWATAKA