Home Uncategorized YANGA YATOA TAMKO KUHUSU SAID NDEMLA WA SIMBA

YANGA YATOA TAMKO KUHUSU SAID NDEMLA WA SIMBA


JUMA Abdul, nahodha msaidizi wa Yanga amesema kuwa anaamini katika uwezo wa nyota wa Simba, Said Ndemla licha ya kwamba hajamuona kwa muda mrefu.

Abdul amesema kuwa miongoni mwa wachezaji ambao amekuwa akiwafurahia wawapo ndani ya uwanja ni pamoja na Ndemla.

“Ni mchezaji mzuri akiwa ndani ya uwanja anajituma na uwezo wake ni mzuri, kwa sasa sijamuona akiwa ndani ya uwanja kwa muda mrefu ila nina amini akipata nafasi atafanya vizuri,” amesema.

Ndemla amekuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu kutokana na ushindani wa namba ndani ya kikosi cha Simba kwenye mzunguko wa pili Simba ikiwa imecheza mechi tisa hajacheza mchezo wowote.

SOMA NA HII  MSIMAMO WA LIGI KUU BARA UPO NAMNA HII