Home Uncategorized FRAGA WA SIMBA HUMUAMBII KITU KUHUSU KUKU, LICHA YA KUPIGWA STOP BADO...

FRAGA WA SIMBA HUMUAMBII KITU KUHUSU KUKU, LICHA YA KUPIGWA STOP BADO WAMO

GERSON Fraga, kiungo wa Simba amesema kuwa wamepigwa stop kula kuku ila akipata muda huwa anafanya hivyo kwa kuwa ni vitu anavyovipenda.

Fraga, raia wa Brazil ametupia mabao matatu kwenye Ligi Kuu Bara kati ya mabao 63 ambayo yamefungwa na Simba.

Kwa sasa Ligi Kuu Bara imesimama kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona.

Fraga amesema: “Kati ya vitu ambavyo ninapenda ni msosi mzuri hasa kuku wa Bongo ni watamu, kwa kuwa tumekatazwa kula sana huwa ninakula pale ambapo ninapata muda kidogo.

“Kila kitu kina uzuri wake na ubaya wake ninatambua umuhimu wa afya ndio maana nimepunguza idadi ya kuku ambao nilikuwa ninakula awali na sasa, mwanzo nilikua nakula kuku wawili mpaka watatu lakini kwa sasa siwezi kula kuku watau ama wawili” .

SOMA NA HII  YANGA YAIFUATA KAGERA SUGAR NA MATUMAINI YA KUTOSHA