MPIANA Mozizi anakipiga ndani ya Klabu ya FC Lupopo inayoshiriki Ligi Kuu nchini Congo.
Timu yake ipo nafasi ya 11 ikiwa imecheza mechi 22 kibindoni ina pointi 24.
Nyota huyo anatajwa kuwekwa kwenye hesabu za klabu za Bongo ambazo zinahitaji kuipata saini yake.
Inaelezwa kuwa Yanga, Azam na Simba zipo kwenye mpango wa kuipata saini yake.