Home Uncategorized IBRAHIM AJIBU ANAFANYA HIVI KULINDA KIPAJI CHAKE

IBRAHIM AJIBU ANAFANYA HIVI KULINDA KIPAJI CHAKE


IBRAHIM Ajibu, kiungo mshambuliaji ndani ya Simba amesema kuwa wakati huu wa mapumziko ya Ligi Kuu Bara kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona amekuwa akichukua tahadhari huku akifanya mazoezi kulinda kipaji chake na kujitoa kwa jamii.

Ajibu amesema kuwa amekuwa akitoa misaada kwa jamii ili kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kupambana na maambukizi ya Virusi vya Corona.

“Nimekuwa nikifanya mazoezi ili kulinda kipaji changu kwani kwa sasa ligi imesimama na hakuna ambacho kinaendelea zaidi ya mazoezi binafsi ambayo kila mmoja anapaswa kufanya.

“Pia nimekuwa nikitoa misaada kwa jamii ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Serikali kupambana na Virusi vya Corona nami nimekuwa nikichukua tahadhari kwa kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima,” amesema.

SOMA NA HII  NYOTA WANNE WA SIMBA WATUA AFRIKA KUSINI, WAANZA KAZI RASMI