GOLIKIPA wa zamani wa timu ya taifa, Taifa Stars, Ivo Mapunda, amemshauri kipa wa Simba, Beno Kakolanya kwenda kutafuta changamoto nje ya nchi ili kulinda kipaji chake alichonacho cha kuokoa michomo golini.
Kakolanya alijiunga na Simba kwenye msimu huu wa Ligi Kuu Bara akitokea Yanga baada ya mkataba wake wa miaka miwili ya kuichezea timu hiyo kumalizika.
Kipa huyo tangu ametua kujiunga na Simba, amekuwa hapati nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo huku akimuachia Aishi Manula ambaye ndio pendekezo la kwanza la Mbelgiji, Sven Vandenbroeck. –
Mapunda amesema kuwa Kakolanya ni kati ya makipa bora nchini ambaye anaamini kama akitoka kwenda kucheza nje ya nchi, thamani yake itaongezeka tofauti na ilivyo hivi sasa.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.