Home Uncategorized MABOSI WA YANGA WAMALIZA UTATA KUHUSU MORRISON

MABOSI WA YANGA WAMALIZA UTATA KUHUSU MORRISON


WANAFAMILIA wa Yanga ambao ni mabosi pia, Kampuni ya GSM imesema kuwa suala lao na Bernard Morrison walishalimaliza hivyo hawana mashaka na nyota huyo kwa sasa.

 Morrison amekuwa kwenye ubora kabla ligi haijasimamishwa kupisha maambukii zaidi ya Virusi vya Corona ambapo kwenye mechi 10 alizocheza amefunga mabao matatu na kutoa pasi tatu za mabao.

Mkurugenzi wa Uwekezaji ndani ya GSM Injinia Hersi Said amesema:”Tumemalizana na Morrison hatuna presha kwani kila kitu kipo sawa na atabaki ndani ya Yanga na taarifa zimeshatolewa.

“Kupitia kwenye ukurasa rasmi wa Istagram wa Yanga, ilielezwa kuwa dili limekamilika na tumemalizana naye kwa kandarasi ya miaka miwili,”.


SOMA NA HII  CR 7 HATMA YAKE NDANI YA JUVENTUS IPO NAMNA HII