Home Uncategorized MANCHESTER UNITED BANA ETI ISHU YA CORONA WAIGEUZA DILI

MANCHESTER UNITED BANA ETI ISHU YA CORONA WAIGEUZA DILI

OLE Gunnar Solskajer, Kocha Mkuu wa Manchester United,amesema kuwa kuibuka kwa Virusi vya Corona kunaweza kuwa na faida kwao kuelekea kwenye dirisha la usajili.


Kwa sasa dunia nzima ipo kwenye janga la kupambana na Virusi vya Corona ambapo klabu nyingi zinapambana kupunguza matumizi ili kuweza kujiepusha na anguko la kiuchumi.


Solskjaer, amedai kuwa, baadhi ya klabu zitalazimika kuuza wachezaji kutokana na kuanguka kiuchumi, hivyo wao kama Man United, wataitumia fursa hii kupata wachezaji wa kiwango cha juu.


Miongoni mwa wachezaji ambao wanatajwa kuwindwa na United ni pamoja na Jadon Sancho, Jack Grealish, Jude Bellingham, Willian na Icard.

SOMA NA HII  IDRSSA GUEYE: ULIKUWA MPANGO WANGU KUTUA PSG, NINA FURAHA KWA SASA