Home Uncategorized TSHISHIMBI: NINAJIFUA KULINDA KIPAJI CHANGU, MUHIMU KUCHUKUA TAHADHARI

TSHISHIMBI: NINAJIFUA KULINDA KIPAJI CHANGU, MUHIMU KUCHUKUA TAHADHARI


PAPY Tshishimbi, kiungo wa timu ya Yanga amesema kuwa kwa sasa anaendelea kulinda kipaji chake ili kuwa bora pale ligi itakaporejea.

Nahodha huyo wa Yanga amesema kuwa anaamini iwapo kila mmoja atachukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona pamoja na kuomba dua mambo yatakuwa sawa na kila kitu kitarejea kwenye hali yake.

“Kikubwa kinachotakiwa kwa sasa ni kila mmoja kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona nina amini mambo yatakuwa sawa bila kusahau kufanya dua.

“Muda huu ninautumia kufanya mazoezi binafsi pamoja na kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Corona.”.

SOMA NA HII  STRAIKA HATARI ORLANDO PIRATES KUTUA SIMBA, AAGA RASMI