Home Uncategorized HIZI HAPA ZILIZOTINGA HATUA YA ROBO FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO

HIZI HAPA ZILIZOTINGA HATUA YA ROBO FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO


SHUGHULI za michezo zinatarajiwa kurejea rasmi Juni Mosi ambapo mechi zilizobaki zitachezwa kwenye vituo viwili, Dar es Salaam na Mwanza.

Mechi zile za Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho zote zitapigwa Dar huku zile za Ligi Daraja la Kwanza na la Pili zikipigwa Mwanza.

Hizi hapa timu zilizoingia robo fainali kwenye Kombe la Azam Sports ni Simba, Yanga, Azam FC, Kagera Sugar, Alliance, Ndanda, Sahare All Stars na Namungo.

Mabingwa watetezi ni Azam FC ambao waliitungua kwa mbinde Ihefu ya Mbeya ambayo ipo Ligi Daraja la Kwanza.

Kwenye timu zilizotinga hatua ya robo fainali ni Sahare All Stars pekee inashiriki Ligi Daraja la Kwanza nyingine zote zipo kwenye ligi.

SOMA NA HII  NIYONZIMA,TSHISHIMBI NA MARRISON WAWEKWA MTEGONI YANGA..!!