Home Uncategorized MAKAMBO NA YANGA MAMBO FRESH SASA

MAKAMBO NA YANGA MAMBO FRESH SASA


BAADA ya Klabu ya Yanga kudaiwa kuwa kwenye harakati za chini kwa chini za kumrejesha straika wao wa zamani raia wa DR Congo, Heritier Makambo, hatimaye dili hilo limetiki baada ya timu ya Horoya AC kukubali kumuachia nyota huyo.
Makambo aliachana na Yanga mwishoni mwa msimu uliopita baada ya mkataba wake kumalizika, kisha akatimkia nchini Guinea ambapo alisajiliwa kwa mkataba wa miaka mitatu kuitumikia Horoya AC.
Habari zinaeleza kuwa baada ya uongozi wa Yanga kuwa kwenye mazungumzo ya muda wa kuwashawishi mabosi wa Horoya AC, ili wamrejeshe nyota wao huyo, hatimaye mambo yamekaa sawa baada ya uongozi huo kukubali kumuachia ajiunge nao kwa miaka miwili.

“Naomba nikuibie siri tu kwamba, siku si nyingi tunaenda kuwashanganza wale wote waliokuwa wakidhani hatutaweza kumpata Makambo, eti kutokana na timu yake kuhitaji dau kubwa kiasi cha wengi kujikuta wakisema Yanga haitaweza kumrejesha ila kwa taarifa tu ni kwamba muda wowote kuanzia sasa mambo yataanikwa.
“Wale ndugu zetu wa Horoya, ni kweli kwamba hawakutaka kabisa kumuachia Makambo, ila viongozi wenzangu wamepambana vya kutosha kiasi cha kujikuta wakiwalainisha na kubaki wakituomba watupe kwa mwaka mmoja japo tumewataka nasi watusikilize zaidi na tayari wameelekea kukubali kumuachia rasmi ambapo atasaini miaka miwili,” kilisema chanzo hicho.

Makambo amekuwa akitajwa kuwa chaguo namba moja kwenye usajili ujao wa Yanga na anaaminika kuwa anaweza kufanya mambo makubwa kwenye timu hiyo.

Chanzo:Championi
SOMA NA HII  HIZI HAPA LEO TIMU 14 UWANJANI KUSAKA POINTI TATU