Home Uncategorized MTUPIAJI WA ZAMANI WA YANGA TAMBWE ATAMANI KURUDI TENA KIKOSINI

MTUPIAJI WA ZAMANI WA YANGA TAMBWE ATAMANI KURUDI TENA KIKOSINI

AMIS Tambwe raia wa Burundi

mshambuliaji wa zamani wa Yanga amesema kuwa anatamani kurudi kukipiga  ndani ya klabu hiyo.

Tambwe alijiunga na Yanga msimu wa 2014/15 baada ya kupigwa chini na Simba aliachwa na Yanga msimu wa 2018/19 na alitimka mpaka Oman ila kwa sasa ni mchezaji huru.

Tambwe amesema:”Miongoni mwa timu ambazo zimenipa heshima ni Yanga sina cha kuwalipa zaidi ya kufanya nao kazi tena kwa mafanikio mengine. “Nikipata nafasi ya kurudi nitafurahi na nitafanya kazi kwa juhudi ninapenda kuwa pale mpaka nitakapostaafu maisha yangu ya  soka.” Msimu aliosepa Tambwe alitupia mabao 12 ambapo 8 alifunga kwenye ligi na manne alifunga kwenye Kombe la Shirikisho.

SOMA NA HII  UJUMBE HUU WA ALLIANCE WATUMWA YANGA