Home Uncategorized HUYU HAPA MRITHI WA JOHN BOCCO

HUYU HAPA MRITHI WA JOHN BOCCO


NAHODHA wa Simba, John Bocco alikuwa wa kwanza kufunga bao  kwenye Uwanja wa zamani wa Azam Complex Chamazi, Agosti 20,2011 mbele ya Moro United.

Bocco alifunga bao hilo kwa penati dakika ya 45, baada ya Bocco mwenyewe kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari.

Bao la kwanza kwenye uwanja mpya wa Azam Complex, Chamazi, limefungwa na Richard Djodi ambaye amerithi mikoba ya Bocco ambaye kwa sasa anakipiga ndani ya Simba ilikuwa ni kwenye mchezo dhidi ya Mbao FC.

Ni katika mchezo wa kwanza wa ligi baada ya mapumziko ya miezi mitatu ya Corona, uliochezwa Juni 14, Azam FC ikishinda mabao 2-0.

SOMA NA HII  HUYU HAPA NYOTA ANAYEKIPIGA TIMU YA TAIFA YA RWANDA ANAYEWINDWA NA YANGA