Home Uncategorized MWADUI,YANGA ZAPEWA TANO NA TFF KWA KUFUATA MUONGOZO WA SERIKALI

MWADUI,YANGA ZAPEWA TANO NA TFF KWA KUFUATA MUONGOZO WA SERIKALI

MASHABIKI wa Mwadui na Yanga leo wamfuata muongozo uliotolewa na Serikali kwa kukaa umbali wa mita moja ikiwa ni tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona.

Mchezo wa leo Juni 13 ni wa Ligi Kuu Bara ambao unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na timu zote kuwa na uhitaji wa pointi tatu.

Shirikisho la Soka Tanzania,(TFF) limewapongeza mashabiki wote kwa kufuata muongozo uliotolewa na Serikali.

Serikali imeridhia masuala ya michezo kuendelea huku ikiwataka wadau wa michezo kuzingatia tahadhari za Corona kwa kuwa janga hili bado lipo.

SOMA NA HII  Wachezaji waliokamilisha usajili Ligi Kuu 2019/20