Home Uncategorized SIMBA INA MATUMAINI KIBAO KUFIKIA MALENGO YAKE

SIMBA INA MATUMAINI KIBAO KUFIKIA MALENGO YAKE


KOCHA Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck amesema kuwa bado ana imani na kikosi chake licha ya kuambulia sare mbele ya Ruvu Shooting.

Simba, Juni 14 ilibanwa mbavu na Ruvu Shooting kwenye mchezo wake wa 29 kwa kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 Uwanja wa Taifa, kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara.

Jana iliibamiza Transit Camp mabao 4-0 kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa Uwanja wa Uhuru, inajiandaa na mchezo dhidi ya Mwadui FC utakaopigwa Juni 20, Uwanja wa Taifa.

Sven amesema:”Bado kuna matmaini ya kufanya vizuri, wachezaji wanaonyesha wana jambo ambalo wanalo itawafanya waendelee kupambana kutafuta matokeo.”

Simba ipo nafasi ya kwanza kibindoni ina pointi zake 72 ikiwa imetupia jumla ya mabao 64.

SOMA NA HII  Wakimataifa ni wanne msimu wa 2019/2020