Home Uncategorized YANGA YAIPOTEZA KAGERA SUGAR KWENYE TAKWIMU, SASA INAONGOZA LIGI

YANGA YAIPOTEZA KAGERA SUGAR KWENYE TAKWIMU, SASA INAONGOZA LIGI

 


YANGA leo Septemba 19 imeibuka na ushindi wa bao 1-0 mbele ya Kagera Sugar kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Kaitaba, Bukoba.

Bao pekee la ushindi lilifungwa na Tonombe Mukoko dakika ya 72 kwa pasi ya Tuisila Kisinda ndani ya 18.

Ushindi huo unaifanya Yanga kuwa nafasi ya kwanza kwenye msimamo baada ya kufikisha jumla ya pointi saba kibindoni na imefunga jumla ya mabao matatu.

Kagera Sugar ni mchezo wake wa pili kupoteza ikiwa Uwanja wa Kaitaba kwa kuwa mchezo wake wa ufunguzi ilifungwa bao 1-0 mbele ya JKT Tanzania Uwanja wa Kaitaba na leo imefungwa bao 1-0 mbele ya Yanga.

Hizi hapa takwimu za mchezo wa leo:-


SOMA NA HII  JUMA ABDUL, YONDANI MAMBO SAFI YANGA, DANTE MAMBO BADO