Home Simba SC KONDE BOY AREJEA, KUJIUNGA NA KAMBI YA SIMBA

KONDE BOY AREJEA, KUJIUNGA NA KAMBI YA SIMBA


KIUNGO mshambuliaji wa klabu ya Simba, Luis Miquissone ‘Konde Boy’ amewasili rasmi leo jijini Dar es Salaam akitokea nchini Msumbiji, alipokuwa kwa ajili ya mapumziko mafupi na anatarajiwa kujiunga na kambi ya Simba inayojiandaa na mashindano ya Simba Super Cup.

Miquissone alikuwa sehemu ya nyota wa Simba waliopewa ruhusa ya kwenda kupumzika baada ya timu hiyo kufanikiwa kutinga hatua ya makundi ya Ligi ya mabingwa Afrika ambapo Simba iliiondosha FC Platimun kwa ushindi wa jumla ya mabao 4-1.

Miquissone aliyehusika kwenye mabao nane ya Simba akifunga bao moja na kuasisti mara saba kwenye michuano ya Ligi Kuu Bara, alikosekana katika michuano ya kombe la Mapinduzi iliyomalizika kwa Yanga kuibuka na ubingwa baada ya kuifunga Simba kwa changamoto ya mikwaju ya Penalti 4-3.

Michuano ya Simba Super Cup itakayoshirikisha timu tatu za Simba, TP Mazembe na Al Hilal inatarajiwa kuanza kutimua vumbi kesho kwenye uwanja wa mkapa ambapo Simba wataianza karata yake kwa kucheza dhidi ya Al Hilal ya Sudan.

SOMA NA HII  HUYU HAPA STARIKA MWILI JUMBA ANAYEKUJA KUCHUKUA NAFASI YA KAGERE MSIMBAZI