Home Azam FC WAKATI WADAU WAKIDHANI AZAM IMEFUFUKA…KOCHA WAO MSOMALI AGUNA KISHA AKASEMA HAYA…

WAKATI WADAU WAKIDHANI AZAM IMEFUFUKA…KOCHA WAO MSOMALI AGUNA KISHA AKASEMA HAYA…


AZAM inakamata nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara lakini kocha wake, Abdi Hamid Moalin, amesema bado hajaipata Azam anayoitaka na ubora wa kikosi chake kwa sasa hauzidi asilimia 65.

Moalin amefunguka kuwa kuna levo ya ubora ambayo anahitaji kuiona kwenye timu yake, jambo ambalo bado analifanyia kazi kwa sasa na atafanikiwa muda siyo mwingi.

“Timu inapata matokeo ya ushindi mfululizo, ila kwetu bado hatujafikia kwenye kiwango ambacho tunahitaji timu icheze na idumu kwenye ubora huo. Nafikiri (kwa sasa) ni kama asilimia ni 55 au 65 tu,” alisema.

Azam imeshinda mechi tatu mfululizo za Ligi Kuu Bara, haijapoteza mechi yoyote tangu ifungwe na Simba 2-1 siku ya Mwaka mpya.

SOMA NA HII  KUHUSU ISHU YA 'KUVIMBA KICHWA'...KABUNDA AFUNGUKA A-Z NAMNA NAMUNGO WANAVYOISHI NAYE...