Wakiwa na kazi ya kusaka ushindi kwenye mchezo dhidi ya Raja Casablanca, mikoba ya nahodha msaidizi wa Simba, Mohamed Hussein Zimbwe Jr inatarajiwa kuwa mikononi mwa Gadiel Michael.
Zimbwe atakosekana kwenye mchezo huo unaotarajiwa kuchezwa Aprili Mosi, mwaka huu ikiwa ni mchezo wa hatua ya makundi kwa timu hizo mbili ambazo zimetinga robo fainali Ligi ya Mabingwa Afrika.
Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally, alisema kuwa watakosa huduma ya Zimbwe kutokana na adhabu ya kadi za njano, lakini wachezaji wengine wapo tayari.
“Tutakosa huduma ya nahodha msaidizi Mohamed Hussein, lakini wapo wachezaji wengine wapo tayari kutokana na mbinu za mwalimu mwenyewe atakavyoamua kuanza.
“Tukiwa ugenini hatuna hofu kwani licha ya kwamba tumetinga hatua ya robo fainali mchezo wetu dhidi ya Raja Casablanca ni muhimu kupata matokeo mazuri, tutafanya jitihada kubwa kupata matokeo chanya,” alisema.