Home Habari za michezo KWA YANGA HII WAPINZANI TUMBO JOTO, ALLY KAMWE ATAMBA

KWA YANGA HII WAPINZANI TUMBO JOTO, ALLY KAMWE ATAMBA

Afisa Habari wa Yanga SC Ally Kamwe

Afisa habari wa klabu ya Yanga Ali Kamwe amesema kile walichokifanya katika mchezo dhidi ya Magereza ni kionjo tu na inamaanisha Yanga ya Gamondi itakua ikifunga magoli kama Mvua.

Yanga walicheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Magereza na kuifunga goli 10-0 katika mchezo wa kujiweka sawa kuelekea mchezo wa kwanza wa ngao ya Hisani dhidi ya Azam FC.

Kabla ya mchezo dhidi ya Aam Yanga wanatarajia kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Klabu ya AS Vita ya Congo Agosti 6.

SOMA NA HII  UNAAMBIWA HUKO JANGWANI NI MWENDO WA SUPU TU ....... HERSI ATOA CHAPATI 5000