Home Habari za michezo YANGA HAKUNA KUPOA WATINGA KAMBINI KUWAWINDA SIMBA

YANGA HAKUNA KUPOA WATINGA KAMBINI KUWAWINDA SIMBA

Habari za Yanga

Kikosi cha Yanga SC, kesho Jumatatu, Oktoba 30, 2023 jioni kinatarajiwa kuanza mazoezi kuelekea Dabi ya Kariakoo.

Mchezo huo wa Ligi Kuu ya NBC ambao umepangwa kuchezwa Jumapili ijayo ya Novemba 5, 2023, tutakabiliana na Simba kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar Es Salaam.

Yanga tutaingia kwenye mchezo huo ikiwa vinara katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC tukifikisha pointi 18, huku tukifunga magoli 20 na kuruhusu magoli 4.

SOMA NA HII  BUMBULI HAJARIDHIKA NA MAAMUZI YA KUFUNGIWA,SIMBA WATOA NENO