Home Habari za Yanga Leo SILAHA YA AZIZ KI NI HAPA…KILA KITU KITAJULIKANA

SILAHA YA AZIZ KI NI HAPA…KILA KITU KITAJULIKANA

Habari za Yanga leo

KIUNGO Mshambuliaji wa Yanga na Mfungaji bora wa Ligi kuu ya NBC AZIZ Ki unaambiwa ujanja wake ndani ya uwanja ni mguu wa kushoto, ambapo unaambiwa kama wewe ni timu pinzani chunga sana unapokutana nae uwanjani haswa akiwa kalitazama goli.

Mbukinabe huyo na staa wa klabu hiyo ametumia zaidi mguu wake wa kushoto katika kupachika nyavuni mipira, kwa kupiga mashuti yake au kwa kutumia ufundi mwingi kwani ndio mguu aliotumia kuambao kufunga mabao mengi zaidi.

Ipo wazi kuwa msimu wa 2023/24 Aziz Ki ni kinara namba moja kwa utupiaji, akiwa katupia mabao 21 baada ya msimu kugota mwisho akiwa ni mfungaji bora.

Ujanja wake akiwa uwanjani ni kwenye mguu wa kushoto ambapo kafunga jumla ya mabao 17 akitumia mguu huo kuwaadhibu wapinzani.

Ikumbukwe kwamba Yanga ni mabingwa wa ligi kuu wa NBC wakiwa namba moja kwenye msimamo na pointi zao ni 80.
Ki ni chaguo la kwanza la Kocha Mkuu Miguel Gamondi ambapo alifunga bao moja kwa pigo la kichwa ilikuwa mchezo dhidi ya Tabora United uliochezwa Uwanja wa Mkapa.

Mabao matatu (3) kafunga kwa mguu wa kulia nyota huyo ambaye mkataba wake umeisha mwisho msimu huu, lakini inasemekana yupo kwenye mazungumzo na mabosi wa Yanga kuongeza kandarasi nyingine.

Hivi karibuni Aziz Ki alitangaza kuwaaga mashabiki na viongozi wa klabu hiyo, huku akiwashukuru kkwa mkuwa namsimu bora zaidi wakifanikiwa kutwaa mataji muhimu yandani, kama Kombe la Ligi Kuu, na Kombe la Shirikisho la CRDB kwa mara ya pili mfululizo.

SOMA NA HII  AZIZ KI AFUNGUKA "UCHAWI" ULIOMFANYA ARUDI 'MJINI' NA YANGA MSIMU HUU...