KLABU ya Simba SC imeshakamilisha kandarasi ya beki wa kushoto wa Coastal Union Lameck Lawi, ambaye kila kitu kipo tayari anasubiri tu kutambulishwa.
Lameck Lawi msimu uliomalizika alikuwa na kiwango bora sana kwa WAGOSI wa Kaya, Coastal Union ambao ameisaidia timu yake kumaliza katika nafasi ya 4 ya Ligi kuu na kuifanya ishiriki kombe la shirikisho Afrika.
Simba ilifanya mazungumzo na mchezaji huyo, na kisha kumsajili ambapo inadaiwa wamempa mkataba wa miaka miwili na mshahara mnono.
Lengo la kufanya usajili huo, Uongozi wa Simba unahitaji kutafuta mbadala na beki wao wa kushoto, Mohammed Hussein ambaye ametumika sana kwa misimu mingi, tena akiwa na kiwango bora zaidi.
Sasa basi, nao Coastal Union wamejibu mapigo kwa kuuliza uwezekano kumnasa beki wa Simba, Kennedy Juma kwa mkataba wa mkopo wa mwaka mmoja.
Kennedy Juma amekuwa mhimili mzuri wa klabu ya Simba katika safu ya ulinzi, baada ya Henock Inonga kuumia kwenye mchezo dhidi ya Tanzania Prisons, akapona akaja kuumia tena kwenye mcheezo wa Dabi kipindi cha kwanza tu, ambapo Simba ilipoteza kwa magoli 2-1.