Straika wa zamani wa Simba, Freddy Michael ambaye alikuwapo uwanjani akiishuhudia timu yake ya zamani ikimkanda Mwarabu mabao 3-1 na kufuzu hatua ya makundi ya michuano ya Kimataifa kwa jumla ya mara 6.
Freddy alisema licha ya ushindi, lakini amekoshwa na Ateba, huku akiitabiria kufika mbali.
“Nimekuja kuangalia mechi, nimekuja kuwaona rafiki zangu, unajua kwenye kikosi nina marafiki zangu wengi sana.
“Simba imecheza vizuri, imeshinda, ina wachezaji wazuri, imesajili wachezaji wengi wenye ubora, Ateba ni straika mzuri na amefunga, nadhani wataenda kufanya vizuri msimu huu, nawatabiria fainali,” alisema.
[…] Leonel Ateba ni mshambuliaji mzuri, ndani ya mechi chache ameonesha kiwango murua sana na kuisaidia timu yake kwenye upatikanaji wa matokeo mazuri. […]
[…] Leonel Ateba ni mshambuliaji mzuri, ndani ya mechi chache ameonesha kiwango murua sana na kuisaidia timu yake kwenye upatikanaji wa matokeo mazuri. […]