Home Habari za Simba Leo KIPINDI CHA KWANZA SIMBA WANASHINDANA KUKOSA MAGOLI.

KIPINDI CHA KWANZA SIMBA WANASHINDANA KUKOSA MAGOLI.

Ni kama tu Simba kule kwenye eneo la mbele wanashindana kukosa nafasi za kufunga, Ateba nafasi tatu zote kashindwa kufunga, kwa aina ya “profile” na alichokifanya dhidi ya Azam mchezo uliopita alipaswa kuipa Simba walau bao moja kwenye kipindi cha kwanza.

Kijili bado hana maamuzi mazuri kwenye eneo la mwisho ambalo ndilo la msingi kuliko kawaida,bado Ahoua hajawa na mchezo mzuri, uwepo wa washambuliaji wawili, in numbers Simba wnakakuwa wachache mbele hali inayomfanya Debora muda mwingi kusogea mbele kuongeza nguvu na idadi kubwa ya wachezaji wa Mnyama.

Kibu katika eneo la Kijili kama tu amejimilikisha,baada ya kumkimbia Zimbwe eneo la kushoto huku kulia anajifanyia kile anachotaka,bado Simba Simba hawana utulivu kwa ujumla eneo la mwisho.

Dodoma wameamua kwenda tofauti na matarajio ya Simba,wameamua kupishana nao tofauti na timu nyingi za mikoani ambavyo huwa zinakuwa second dhidi ya timu za Kariakoo !!

HT” || DOM 0-0 SIMBA

SOMA NA HII  BAADA YA KUKIWASHA MECHI YA DAR....NTIBAZONKIZA AWALIA KIAPO AL AHLY MECHI YA MISRI...

1 COMMENT

  1. […] ya Simba imeshinda mchezo wake wa pili wakiwa ugenini kwa bao 0-1 dhidi ya wenyeji Dodoma […]

Comments are closed.