Home Habari za Simba Leo BAADA YA MPANZU… ANAYEFUATIA SIMBA NI FEI TOTO

BAADA YA MPANZU… ANAYEFUATIA SIMBA NI FEI TOTO

habari za simba

Mnyama Simba Sports Club, Feisal Salum ‘FEITOTO’ ndiye mchezaji ambae yupo kwenye Target yao, mahitaji yao ni kumpata dirisha dogo la usajili la usajili na mazungumzo yameshaanza.

Simba ipo tayari kulipa kilichopo kwenye mkataba wa Feisal Salum ili ajiunge Simba Sports Club.

MO Dewji na Salim Abdallah Muhene ‘Try Again’ wapo tayari kukamilisha uhamisho wa Feisal Salum.

Hadi sasa Fei Toto bado hajakubali kuongeza mkataba mpya na Azam FC, licha ya Uongozi wa timu hiyo kumpatia mkataba mpya ili asaini na aendelee kuitumikia Azam FC.

Malengo ya Fei Toto ni kucheza timu kubwa yenye uhakika wa kucheza mechi za Kimataifa, hivyo hii huenda ikawa ni urahisi wa Simba kumpata mchezaji huyo hatari mwenye uwezo mkubwa wa kufunga, kwa aina yeyote ile.

SOMA NA HII  HATMA YA RUFAA YA MAGOMA KUJULIKANA SEPTEMBA 9

1 COMMENT

  1. […] mechi chache za AS Vita msimu uliopita akiwepo Elie Mpanzu, sio sababu yoyote kwanini asiwe tatizo / hatari kwa wapinzani katika michuano ya ndani hadi nje, […]

Comments are closed.