Nilishuhudia mechi chache za AS Vita msimu uliopita akiwepo Elie Mpanzu, sio sababu yoyote kwanini asiwe tatizo / hatari kwa wapinzani katika michuano ya ndani hadi nje, anasaidia kuboresha / vitu vingi kwa timu yako ( Simba ) / winga yako
-
Mchezaji ambaye amebarikiwa sana ufundi miguuni ( zile touch zake, one touch football na ile combination play , kwa maana anakupa leseni ya kucheza eneo finyu na kushinda mipambano )
-
Mchezaji ambaye anacheza huku macho yanaangalia juu ( sio yule mchezaji ambaye anafanya runs zake / kusprint akiwa macho sini muda mwingi ) , kitendo hicho kinamfanya aweze kuziona pasi na kuzipiga, gifted player.
-
Kasi nzuri inahitajika kwa Mshambuliaji wa pembeni na kuingia ndani ( yani yupo explosive mithiri ya Vini Jr, Rashy , Saka, Dembele na Diaz ) , kwa maana inampa leseni ya kufika katika actions / mpinzani kwa nyakati sahihi.
-
He can score goals and create them ( anajua kutengeneza nafasi za mabao, na mmaliziaji mzuri tu, yes he can see a pass, keep the ball )