Home Uncategorized KUKAMATWA KWA MZEE KILOMONI KWAWA GUMZO…

KUKAMATWA KWA MZEE KILOMONI KWAWA GUMZO…

Kukamatwa kwa mwanachama maarufu wa Simba, Hamisi Kilomoni kutokana na kufanya mkutano wa waandishi wa habari bila ya kuwa na kibali, imezua gumzo kubwa.

Katika mitandao wad wamekuwa wakijadili kuamini kuwa ameonewa, lakini wapo wamekuwa wakiwaelewesha wenzao kuhusiana na utaratibu wa kutakiwa kuwa na kibali kabla ya kufanya mkutano na waandishi.


Kilomoni amekatwa leo asubuhi nyumbani kwake Kinondoni Block 41 jijini Dar es Salaam wakati akijiandaa kufanya mkutano na waandishi wa habari.

Baadhi ya wadau wamekuwa wakiamini kukamatwa kwake kumetokana na fitna za soka. Lakini wengine wamesisitiza kufuatwa kwa sheria na kukosea na baadaye suala la fitna ndio liwe kisingizio.
SOMA NA HII  NAMUNGO YAPANIA KUTUSUA KESHO MBELE YA WASUDAN