Home Uncategorized SABABU ZA SIMBA KUREJEA KESHO HIZI HAPA

SABABU ZA SIMBA KUREJEA KESHO HIZI HAPA

CRESCENTIUS Magori, Ofisa Mtendaji Mkuu wa klabu ya Simba amesema kuwa jeshi kamili la Simba linatarajiwa kurejea kesho kutoka Afrika Kusini kwa ajili ya maadalizi ya mwisho ya mchezo wao wa kirafiki pamoja na ule wa kimataifa.

Kikosi cha Simba kimeweka kambi nchini Afrika Kusini kwa ajili ya maandalizi ya Ligi Kuu Bara pamoja na michuano ya kimataifa.

Magori amesema:”Kikosi kitarejea Julai 31 kutoka kambini nchini Afrika baada ya kumaliza ratiba ya maandalizi ya michuano ya kimataifa pamoja na Ligi Kuu Bara.

“Wanarejea kwa ajili ya kazi moja kuendeleza moto wa Simba kuelekea Simba day na maandalizi ya mwisho kwenye mchezo wetu wa kirafiki dhidi ya Power Dynamo, na ule wa kimataifa dhidi ya UD Songo” amesema.

SOMA NA HII  MAMBO MAGUMU KWA SAID NDEMLA NDANI YA SIMBA